الاثنين، 17 أبريل 2017

HIKI NI KITABU CHENU WENYEWE KISOMENI MSISUBIRI KUSOMEWA

HIKI NI KITABU CHENU WENYEWE KISOMENI MSISUBIRI KUSOMEWA
Kumbukumbu la Torati 16:1
[1]Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka BWANA, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku BWANA; Mungu wako.
Je huu Mwezi wa ABIBU ni Mwezi gani....? Na ikiwa PASAKA imefanyika kwenye Mwezi wa ABIBU kabla ya Kuzaliwa kwake YESU. Je Khitmah ya YESU ilianza Kusherehekewa kabla ya Kuzaliwa kwake....?
YESU Mwenyewe pia Amesherehekea Sikukuu ya PASAKA Je Alijitabiria Kifo Chake....?
Luka 2:41-42
[41]Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka.
[42]Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu;
👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇
JE MFU ANAFUFUKA.....?
1 Wakorintho 15:15-18
[15]Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
[16]Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.
[17]Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.
[18]Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.
KAMA KILA AANGIKWAE JUU YA MTI AMELAANIWA. JE YESU PIA AMELAANIWA...?
Wagalatia 3:13
[13]Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
NA JE YESU KABLA YA KUSULUBIWA ALIVIKWA VAZI LA RANGI GANI....?
Yohana 19:5
[5]Ndipo Yesu alipotoka nje, naye amevaa ile taji ya miiba, na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, Tazama, mtu huyu!
Mathayo 27:28
[28]Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::
************************************************
وَقَالُوا كُونُوا هُودًا أَوْ نَصَارَىٰ تَهْتَدُوا ۗ قُلْ بَلْ مِلَّةَ إِبْرَاهِيمَ حَنِيفًا ۖ وَمَا كَانَ مِنَ الْمُشْرِكِينَ
Na wakasema: Kuweni Mayahudi au Wakristo ndio mtaongoka. Sema: Bali tunashika mila ya Ibrahim mwongofu, wala hakuwa katika washirikina.
{Baqara 135}
وَجَاهِدُوا فِي اللَّهِ حَقَّ جِهَادِهِ ۚ هُوَ اجْتَبَاكُمْ وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ ۚ مِلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ ۚ هُوَ سَمَّاكُمُ الْمُسْلِمِينَ مِنْ قَبْلُ وَفِي هَٰذَا لِيَكُونَ الرَّسُولُ شَهِيدًا عَلَيْكُمْ وَتَكُونُوا شُهَدَاءَ عَلَى النَّاسِ ۚ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَاعْتَصِمُوا بِاللَّهِ هُوَ مَوْلَاكُمْ ۖ فَنِعْمَ الْمَوْلَىٰ وَنِعْمَ النَّصِيرُ
Na fanyeni Juhudi kwa ajili ya ALLAAH kama inavyo stahiki jihadi yake. Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim. Yeye (ALLAAH) alikuiteni Waislamu tangu zamani, na katika hii (Qur'aan) pia, ili awe Mtume shahidi juu yenu, na nyinyi muwe mashahidi kwa watu. Basi shikeni Sala na toeni Zaka na shikamaneni na ALLAAH. Yeye ndiye Mlinzi wenu, Mlinzi bora kabisa, na Msaidizi bora kabisa.
{Hajj 78}
أعجبني
تعليق

ليست هناك تعليقات:

إرسال تعليق